Wednesday, July 2, 2014

KAMA ANN ANNIE NASEMA MBEYA GOSPEL FESTIVAL 2014 HAISIMULIKI...

Mimi kama Ann Annie ninamshukuru Mungu kwanza kwa kuniwezesha kushiriki katika Tamasha kubwa sana jijini Mbeya linaloenda kwa jina la Mbeya Gospel Festival. Niliweza kuuona utukufu wa Mungu kwa kupitia uimbaji wa wenzangu niliokuwa nao katika tamasha hili la kipekee.

Tamasha hili lilihudhuria na watu wengi sana ambapo nilishindwa kushangaa na nikabaki mdomo wazi. Nilichojifunza ni kwamba kumbe watu wanaohitaji Injili ni wengi lakini watenda kazi ni wachache.

Tamasha hili liliandaliwa na Chama Cha Muziki wa Injili Tanzania kwa lengo la kuwahimiza wakazi wa mkoa wa Mbeya kujiunga na chama hicho ili waweza kujua haki zao za Muzikia na pia kuleta mshikamano na ushirikiano kati ya waimbaji.

 kushoto ni Ann Annie

Ann Annie akifanya mambo kwa utukufu wa Mungu

 Ann Annie katikati na waimbaji wenzake (kulia ni Rachel Sharp)
 Rachel Sharp
 Emmanuel Mabisa
 Mwasomola
 Mess Jacob Chengula aliyevalia koti jeupe


No comments:

Post a Comment